Tuesday, 16 February 2016

Ladha ya Penzi (The Taste Of Love) Sehemu ya Tatu.


“Inna my girl! Najua mimi ni msichana na usichana wangu haunizuii kupenda wala kupewa raha wapatazo wanaume” aliongea Solidad kwa kijiamini sana. “Sikia Solidad msichana yeyote aliyakamili kamwe hawezi fanya haya mabo unayotaka kufanya” Inna aliongea akigeukia upande wa pili nakukumbatia mto. “No! usiseme hivyo nahisi mimi ni msichana ambaye sijakamilika kuitwa msichana kwa sababu mbili …….. Moja sina hisia na mwanaume yeyote duniani, pili nina hisia za kimapenzi na wasichana wazuri kama wewe na hata kakazangu wanalitambua hilo na moja kwa moja wanaelewa wewe ni mpenzi wangu but Sorry Inna” aliongea solidad kwa Uchungu uliopitiliza na kumfanya Inna arudishe sura yake upande wake. 
Tendo hilo lilimpa faraja kubwa sana Solidad. “Solidad stop saying that! What kind of a girl are you?” (Solidad acha kuongea ivyo wewe ni msichana wa aina gani?) Inna aliongea akionyeshwa kushangazwa na maneno ya soledad “Nipatie chance Inna nitakuonyesha kwamba najua kumhendo mschana vilivyo” alisema solidad kwa kujiamini. “But solidad don’t you know that I have a boy?” (lakini Solidad hujui kuwa nina mwanaume?) Inna alimuuza Solidad. “Najua lakini sio chanzo cha yeye kunizibia na ninajua mnapendana sana na Castro, hakuna asiyelijua hilo lakini nipatie chance nami nikuonyeshe mapenzi niliyo nayo kwako”

Castro ni kijana mtanashati anayefanyakazi kwnye kampuni ya Multichoice Tanzania inayohusika na Usambazaji wa vifaa vya DSTV pamoja na urushaji wa matangazo kwenye Television. Ni mwanaume na  kijana wa kipekee aliyempenda sana Inna kwa moyo wake wote na wazazi wao pande zote mbili walilitambua hilo, “Inna ndiye msichana nitake muoa mimi hakuna mwingine” Castro alipenda kuyarudia maneno hayo kila anapomkumbuka Inna.

Solidad na Inna walibaki wakijibizana mpaka ilipohitimu saa nane usiku, Inna aliemdelea kuonyesha msimamo aliokuwa nao, na Solidad alijitahidi kumbembeleza jinsi awezavyo, ikafikia kipindi Inna akajuta kumjua solidad na zaidi sana kukanyaga nyumbani kwao, lakini kwa nguvu ya mapenzi aliyokuwa nayo Solidad aliweza kumshawishi Inna, nae akajikuta anazama katika penzi la msichana solidad”

Mke wangu mpaka wakati huu uyu mtoto hajafika bado” mzee Ambachi alikuwa akimuuliza mke wake. “mume wangu na mimi hata sielewi tatizo ni nini lakini ngoja nipigie simu” aliongea mama Ambachi akitoa simu yake na tayari kwa kupiga.

Inna alionekana akiwa kwenye dimbwi la mawazo mara ghafla alishtuliwa na sauti a solidad akiingia toka Sebuleni “Baby are you owky?”(aliongea Solidad akimfuata Inna alipokuwa kaketi.
Inna: Ndiyo nipo fresh kabisa
Solidad: Mh! Mbona nakuona uko out of mood please baby tell me what’s up?
Inna: Hapana solidad nipo sawa kabisa hata usijali.
Solidad: Do you love me?
Inna: Yap! Nakupenda Solidad, penzi ulilonipa jana limenifanya nikupende, nisahau hata kurudi nyumbani mapema.
Solidad: usijali Inna, ntakupa mapenzi yote, utamsahau hata huyo Castro wako (aliongea Solidad huku akimkumbatia Inna).

Inna alirudi kwao mchana, kwenye mida ya saa nane, alisindikizwa na solidad, solidad akiwa kwenye usikani. Baada ya kufika nyumbani aliagana na Solidad na moja kwa moja aliingia ndani na kupitiliza chumbani kwake, Alishangaa alipomkuta Castro mpenzi wake akiwa kajilaza kitandani kwake.

“Castro why bila taarifa” Inna aliuliza kwa mshangao
“kwani nikija kwa mke wangu bila taarifa kuna kosa” Castro nae aliuliza. “Hapana Castro unajua umenishtua sana”
Castro: usijali Inna, lakini mbona umechelewa na aliyekushusha na gari hapo nje ni nani?
Inna: Ni rafiki yangu. Anaitwa Solidad na nilikuwa kwao tangu jana.
Castrro: Mh! Uyo ni msichana au mvulana nimeangalia vibaya eee! Na mbona amekuaga kwa kukumbatia kimahaba kabisa.
Inna: (akionyesha ukali) Castro! yule ni rafiki yangu wa kike na hata apa nyumbani wanamfahamu, na kunikumbatia ivyo ndo unashangaa?


Castro: Sorry Inna mke wangu, sijamuangalia vizuri “nilijua ni mwanaume(castro akawa mpole tena kwa Inna). Alimpenda sana lakini upande wa Inna tayari alishachafuka moyoni mwake. Waliongea mabo mengi lakini Inna alikuwa tofauti na siku nyingine zote na Casto alilitambua hilo, Alijaribu kumuuliza Inna tatizo nini lakini Inna hakuweza kumjibu alikuwa tayari kaisha athirika na penzi la Soledad. Inna na soledade waliendela na mapnzi yao na yaliongezeka siku hadi siku.


xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx


Itaendelea Sehemu ya Nne Tafadhili waweza kutoa maoni yako au kushere na marafiki zako
ASANTENI

No comments:

Post a Comment