Wednesday, 24 February 2016

Ladha ya Penzi (The Taste Of Love) Sehemu ya Nne.




ILIPO ISHIA:-

Castro: Sorry Inna mke wangu, sijamuangalia vizuri “nilijua ni mwanaume(castro akawa mpole tena kwa Inna). Alimpenda sana lakini upande wa Inna tayari alishachafuka moyoni mwake. Waliongea mabo mengi lakini Inna alikuwa tofauti na siku nyingine zote na Casto alilitambua hilo, Alijaribu kumuuliza Inna tatizo nini lakini Inna hakuweza kumjibu alikuwa tayari kaisha athirika na penzi la Soledad. Inna na soledade waliendela na mapnzi yao na yaliongezeka siku hadi siku.


    Ni siku ambayo hakuitarajia Inna baada ya matokeo yao kutoka, ilikuwa ishapita kama mwaka mmoja zilitoka post zao ambazo kila mmoja alijitambua anaelekea wapi, Inna hakuamini  baada ya kupangiiwa kwenda uingereza kuendelea na masomo yake kutokana na vigezo vya ufaulu wake kuwa juu zaidi Tanzania nzima. Ilikuwa ni furaha kwake na familia yake tukimtoa Solidad pekee hakuweza kufurahia jambo hilo akiwa na sababu zake za kipekee, walipewa muda wa mwezi mmoja wa kuweza kijiandaa, Inna aliweza kuutumia wakati wote ule kuwa karibu na Solidad wapate kuweza kuagana, hakuwa na muda na Castro na hata wazazi wake walianza kuligundua hilo lakini waliamua kukaa kimya na kubaki kusubiri matokeo yanayofuata juu yao.

Castro aliweza kuligundua hilo lakini aliamua kulifumbia macho na kuwa mpole kabisa kwa Inna akijua alikuwa anatengeneza kumbe alikuwa akiharibu. Hakuwahi kumuona Solidad akiwa karibu yake zaidi ya siku ile alipomuona kamshusha Inna kwenye gari hakuweza kumkariri siku ile na alitamani siku moja amtie Solidad machoni lakini hakupata nafasi hiyo, alikuwa kapania sana kumona Solidad ili amwambie jinsi alivyoumia alihisi yeye angeweza kusaidia kwa sababu alikuwa karibu kabisa na mpenzi wake.

          Siku ya kuondoka kwa inna nchini Tanzania ilitimia, akiwa kwao pamoja na wazazi wake wakijiandaa ili waweze kumpeleka airport, Alitakiwa kuondoka na ndege ya saa saba mchana na wakati huo ilikuwa ni saa nne hasubuhi, tayari Inna kaisha wasiliana na kipenzi chake cha Moyo Solidad Aje amsindikize pamoja na Castro ambaye tayari alikuwa njiani na alikuja kwa mambo mawili, kumsindikiza mpenzi wake na kumuona solidad na alijua moja kwa moja siku hiyo angekuwepo maeneo yale ya Airport. Alijiandaa kikamilifu pamoja na zawadi za mpenzi wake, 

          Kwa wakati huo Solidad alikuwa akifanya kazi kwenye kampuni ya Sabedi Transport na masaa yale alikuwa ofisini kwake. Ofisi yake ilikuwa maeneo ya Sinza. Akiwa mezani kwake simu yake iliita alipoangalia aliona ni jina la kipenzi chake Inna, Alipokea  "hallow baby time zimeenda njoo nyumbani” sauti upande wa pili ilisikia “ohoo! Sorry baby nakuja sasa hivi ngoja nifunge ofisi” alisema Solidad akikusanya mafaili yaliyokuwa mezani kwake. Alikata simu na akaanza kusanya faili zake zote, akatoka na kuanza kufunga ofisi, Mara simu yake tena ikasikika alkuwa ni kaka yake Declease akimtaka aende nyumbani haraka, na kwa maongezi yake aligundua kulikuwa na tatizo aliwasha gari haraka hadi nyumbani kwao alipofika alimkuta declease nje ya nyumba akilia kwa uchungu, alikimbia na kumfua, alimuuliza nini tatizo declease hakuweza kuongea badala yake alibaki akizidi kulia. “Haiwezekani!” Ni maneno aliyotamka declease akiwa analia.

Ilichukua muda kwa decleae kuweza kuongea kilichomfanya awe katika hali ile na Solidad alijitahidi sana kumbembeleza na kumuomba waingie ndani kwa maongezi mazuri. Declease alikubali na wakaingia ndani.

            Declease aliweza kumweleza dada yake juu ya taarifa alizozipata kuhusu kifo cha wazazi wao na aliapa kufuatilia mpaka nchini Canada, Solided aliweza kumweleza kuwa, wazazi wao walishafariki muda mrefu sasa na alimuomba apotezee na ajikaze kwa taarifa alizopaa lakini Declease hakuweza kumsikiliza kwa lolote alilosema.

Ni saa saba kasoro Inna na familia yake pamoja na Castro wakiwa ndani ya gari wakielekea uwanja wa ndege. Inna hakuwa na raha kabisa kutokana na kutokuwepo kwa kipenzi chake Solidad, ameshajaribu kupiga simu ni zaidi ya mara kumi lakini simu haipokelewi, alitamani hata kuhairisha safari yake lakini hakuweza, alitamani arudishe masaa nyuma aweze kumfuata Solidad lakini haikuwezekana alibaki akilia tu safari nzima.


          Walifika maeneo ya airport bila mafanikio ya kuonana na soledad, Inna alilia sana alipoangalia saa yake na ndege ikiwa tayari kwa maandalizi ya safari. Alijikuta anapata hasira alipojaribu kupiga namba ya solidad bila kupokelewa. “Najaribu mara ya mwisho” alijisemea Inna huku akilia, alijaribu tena haikupokelewa alijikuta akilia na kuapata hasira zilizoweza kuonekeana Usoni mwake, Castro alibaki akimwangalia mpenzi wake kwa huzuni alimwona akiandika SmS na kuzima simu yake kwa hasira aliinuka alipokuwa na kumfuata mama yake na kumkumbatia huku akilia, akatoka na kumfuata baba yake na kumkumbatia akimuaga, Castro aliweza kuyashuhudia hayo Inna akarudi akamfuata Castro akamkumbatia huku akilia akasogeza kinywa chake karibu na sikio la Castro akataja herufi ambazo Castro hakuweza kuzielewa “MLWW” ni herufi alizozitamka Inna kwa Castro na kutoka mikononi mwake kwa kasi na kuiwahi ndege.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Itaendelea Sehemu ya Tano Tafadhili waweza kutoa maoni yako au kushere na marafiki zako
ASANTENI

No comments:

Post a Comment