Majira ya saa mbili Solidad pamoja
na rafiki yake mpendwa walitua nyumbani kwao na kuwakuta kaka zake wakiburudika
kwa muziki wa polepole, Solidad na Inna waliingia na kuwasalimu Declease na Clease.
Solidad ni msichana wa pekee katika familia
yao, walizaliwa watatu yaani Clease na Declease
ni kaka zake halafu anafuata yeye, Soledad, clease na Declease ni watoto
chotara walozaliwa na pande mbili yaani Mtanzania na mhindi ni watoto
waliobarikiwa kwa uzuri na akili, Wazazi wao walifariki nchini Canada
kwa ajali ya gari na taarifa za kifo cha wazazi wao kila mmoja alizipata kwa
wakati wake. Solidad ndio alikuwa wakwanza kupata taarifa hizo na hakuweza kumwambia mtu yeyote, na wapili alikuwa ni Clease nae hakumwambia mtu yeyote na
mpaka wakati ule Declease bado alikuwa hajajua taarifa za kifo cha wazazi wao.
Solidad
alibarikiwa kwa uzuri, Sura nzuri na nywele za kishombeshombe alikuwa dizaini kama
mwanaume kwa matendo na nyendo zake, hakuwahi kuvaa sketi wala gauni maisha
yake, kiufupi Solidad hakuwa na Swagger za kike kwa sababu kampani yake kubwa
ilikuwa ni boyz yaani wavulana.
Baada ya salamu, Solidad
alimkaribisha Inna, wakaingia ndani na kuketi, Clease na Declease walionesha mshangao na
walijikuta wanazima muziki na kubaki wakimshangaa Inna, kutokana na uzuri
aliokuwa nao, Solidad aliwaangalia kakaze na akagundua kitu kutoka kwao “ oya
nyie brothers vipi?” alihoji Solidad
“aha! Sister acha zako ina maana hujui”
declease aliitikia. “Sorry, Inna naomba twende ndani tukaongee” Solidad
alimuomba Inna, waongozane hadi chumbani, Inna aliingiwa na uwoga uliosababishwa na maneno ya kaka
zake Solidad aliinuka na kuanza kumfuata Soledad kwa nyuma
wakiwaacha Declease na Clease wakiunguruma na kutoa miguno kwa dada yao
kuwaondolea binti mrembo mbele ya macho yao.
Solidad na Inna waliingia
chumbani na kuketi kitandani “Sorry Inna wale ni kaka zangu na tunaishi watatu
tu humu ndani na hawa wanapenda sana utani So! Naomba uwazoee” alisema Soledad huku mkono wake ukiwa
kwenye Bega la Inna. “usiogope Solidad mbona wapo sawa tu” alijibu Inna
akiinamisha kichwa chini, waliendelea na story za hapa na pale mpaka ilipotimu saa nne na
robo ndipo Inna aliposema anahisi usingizi na kulala akimuacha Soledad akibofya
simu yake na laptop ikiwa mbele yake.
“Nini tena jamani” Sauti ya
Inna ilisikika baada ya kushituliwa na mikono iliyomwingilia katikati ya
matiti yake, "Samahani Inna, I love you” aljibu Solidad kwa saut ya chini na
laini ya kuweza kumtoa nyoka pangoni, Inna alishusha pumzi na kulala tena,
“Solidad what the meaning of this” (Solidad nini maana ya yote
haya?) Inna alihoji kwa upole “I love you!”(nakupenda) Solidad alijibu kwa mkato, “you
are my friend Soledad I know that you love me but think that you are a
girl”(wewe ni rafiki yangu Soledad najua unanipenda lakini fikiria wewe ni
msichana) alisema Inna kwa hisia kali.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
Itaendelea Sehemu ya Tatu Tafadhili waweza kutoa maoni yako au kushere na marafiki zako
ASANTENI

No comments:
Post a Comment